KCMC, EGPAF ZAJADILI AFYA YANGU
Leo, tarehe 7 Septemba 2026, Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini - KCMC imepokea ugeni kutoka Elizabeth Glaser Pediatric AIDS Foundation (EGPAF) Makao Makuu Dar es Salaam na EGPAF Mkoa wa Kilimanjaro, kwa lengo la kutembelea na kujifunza namna KCMC inavyotekeleza huduma zinazohusiana na Mradi wa Afya Yangu (My Health).
Ziara hiyo imelenga kukagua utekelezaji wa Mradi wa Afya Yangu, kubadilishana uzoefu na kuimarisha ushirikiano katika utoaji wa huduma za afya, hususani kupitia Wizara ya Afya na Ofisi ya Waziri Mkuu–TAMISEMI.
Aidha, ugeni huo umelenga kupata uelewa zaidi kuhusu shughuli za mradi zinazotekelezwa KCMC, kutambua mafanikio yaliyopatikana pamoja na kujadili maeneo ya kuendeleza ushirikiano katika kuboresha na kuimarisha huduma za afya.
Related Stories