BANDA LA KCMC LAVUTIA WAGENI ARUSHA
Picha ya kwanza ni Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Afya na Diakonia wa KKKT, Dkt. Zebadiah Paul Mmbando, akiwa miongoni mwa wageni waliotembelea banda la KCMC linalotoa huduma na elimu mbalimbali za afya.
Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini – KCMC imeungana na taasisi mbalimbali zilizo chini ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kutoa huduma na elimu ya afya kwa washiriki wa mkutano unaowakutanisha washiriki kutoka Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Marekani pamoja na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, unaoendelea katika Ukumbi wa Corridor Springs Hotel jijini Arusha.
Kupitia banda lake, KCMC inatoa huduma mbalimbali za afya pamoja na elimu kuhusu magonjwa na namna ya kuyakinga.
Huduma na elimu hiyo zinatolewa kwa siku mbili, zikilenga kuwafikia washiriki mbalimbali wa mkutano huo kwa kuwapa fursa ya kupata maarifa muhimu kuhusu afya pamoja na huduma zinazotolewa na wataalamu wa KCMC.
Related Stories