2026-04-21 00:00:00
•
AFYA
•
5 min read
DKT. URASA AHAMASISHA UPIMAJI WA AFYA
*Leo, tarehe 21 Aprili 2026 - Moshi,*
Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini – KCMC, ukiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Dkt. Sarah Urasa, umezindua rasmi maadhimisho ya siku tano ya Wiki ya Wataalamu wa Maabara za Afya Duniani yanayoendelea hospitalini hapa.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Dkt. Urasa aliwasihi wananchi kujenga utamaduni wa kupima afya zao mara kwa mara ili kutambua mapema changamoto za kiafya na kuchukua hatua stahiki kwa wakati. Alisisitiza kuwa uchunguzi wa mapema unaokoa maisha na kupunguza gharama za matibabu ya baadaye.
Maadhimisho haya yanaendelea hadi tarehe 24 Aprili 2026, yakitoa huduma mbalimbali za uchunguzi wa afya BURE kwa wananchi, pamoja na elimu ya afya na zoezi la uchangiaji damu. Hii ni fursa muhimu kwa jamii kujitokeza, kupata huduma za kitaalamu na kuongeza uelewa kuhusu afya zao.
Tunawahimiza wananchi wote kufika na kunufaika na huduma hizi muhimu.
#KCMC #AfyaKwanza #HudumaBure #MedicalLabWeek #JipimeKwaAfya
Related News