2026-04-21 00:00:00
•
MOYO
•
5 min read
PIGO MOJA LA MOYO NI UHAI
*Aprili 21, 2026 - Dar es Salaam*
Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini – KCMC kwa kushirikiana na Uongozi wa TANLINK umekutana na uongozi wa Benki ya @equitybanktz katika kikao chenye lengo la kujadili namna bora ya kushirikiana katika kuchangia ujenzi wa Taasisi ya Moyo ya KCMC.
Kikao hiki ni sehemu ya jitihada zinazoendelea za kuimarisha huduma za kibingwa hapa nchini kwa kuhakikisha upatikanaji wa miundombinu ya kisasa ya matibabu ya moyo, ambayo itawanufaisha wananchi wa Kanda ya Kaskazini na Tanzania kwa ujumla. Ushirikiano huu unaonesha dhamira ya pamoja kati ya sekta ya afya na taasisi za kifedha katika kuwekeza kwenye afya ya jamii na kuokoa maisha ya Watanzania.
KCMC inaendelea kuwakaribisha wadau mbalimbali kujitokeza na kuunga mkono mradi huu muhimu wa ujenzi wa Taasisi ya Moyo.
#KCMC #TANLINK #EquityBankTanzania #AfyaKwanza #TaasisiYaMoyo #Ushirikiano #BetterHealthcare
https://www.instagram.com/p/DXYt2W8CGU8/?igsh=MWg4b29lNHhmdnBvdg==
Related News