KCMC YATATHIMINI MPANGO MKAKATI 2022-2026
Leo, tarehe 6 Agosti 2026, Uongozi wa KKKT Makao Makuu imefanya kikao na Uongozi wa Shirika la Msamaria Mwema - GSF/KCMC. Kikao hiki kilikuwa na lengo la kutathmini utekelezaji wa Mpango Mkakati wa KKKT wa mwaka 2022–2026.
Kikao hicho kimeongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa KKKT – Mipango na Maendeleo, Bw. Saimon Daffi (wakwanza kushoto), ambapo pamoja na mambo mengine, kimejadili mafanikio, changamoto na hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wa mpango huo, pamoja na maeneo ya kuimarisha ili kufikia malengo yaliyowekwa.
Related Stories